Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Beki wa Singida United atua Simba kumrithi Juuko

63258 Pic+keny

Tue, 18 Jun 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Mabingwa wa Ligi Kuu Bara, Simba wameimalisha safu yao ya ulinzi kwa kumsajili beki wa kati wa Singida United, Kennedy Wilson Juma kwa mkataba wa miaka miwili.

Juma alisaini mkataba kabla ya kwenda kujiunga na kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars kwenye orodha ya wachezaji wa kwanza walioitwa kabla ya kwenda Misri.

Uongozi wa Simba umemsajili Juma ili kuongesa nguvu katika safu ya ulinzi lakini baada ya beki Mganda Juuko Murshid kutangaza kuachana na mabingwa hao.

Nahodha huyo wa Singida United alikuwa katika kikosi cha kwanza Taifa Stars kabla ya kuenguliwa katika orodha ya wachezaji 23 waliokwenda Misri Afcon.

Mwanaspoti wiki iliyopita lilikufichulia usajili wa Juma lilimtafuta na kueleza kwa ufupi kuwa amekuja Simba kushindana ili kuisaidia timu kufikia malengo yake.

"Simba ni timu kubwa nipo tayari kupambana na ushindani ambao nitakutana nao ili kupata nafasi ya kucheza na kuisaidia timu kufikia malengo yake," alisema Juma.

Pia Soma

Chanzo: mwananchi.co.tz