Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Azam imefikia makubaliano na Mholanzi, Hans van der Pluijm

8504 Pluijm.png TZW

Thu, 31 May 2018 Chanzo: bongo5.com

Mkurugenzi wa klabu ya Azam FC, Nassor Idrissa amethibitisha kuwa timu hiyo imefikia makubaliano ya kufanya kazi na Kocha, Hans van der Pluijm tayari kwa msimu ujao wa ligi kuu soka Tanzania Bara na michuano ya kombe la Shirikisho la Azam.



Msimu ujao timu yetu itakuwa chini ya mikono ya Hans van der Pluijm, matarajio yetu ni makubwa sana kwasababu kama ujuavyo mchezo wa mpira huchezwa uwanjani na kila mtu anaona na sisi kama uongozi tunamatarajio makubwa baada ya kuona kazi aliyoifanya Singida kwahiyo tumevutiwa nae sana.

Kwa hiyo tumeona nafasi ipo tumezungumza nae na kwakuwa alikuwa anamaliza kandarasi yake na Singida tumekubaliana tuna matumaini makubwa kwasababu kama klabu tunamalengo ambayo mengine hatuyafikii lakini mengine tunatamani kuyafikia kwahiyo tukiwa na Hans tutafika malengo yetu.

Azam imefikia makubaliano ya kufanya kazi na Hans van der Pluijm raia wa Uholanzi ambaye msimu uliyomalizika imeifundisha klabu ya Singida United kwa mafanikio makubwa baada ya kuifikisho timu hiyo changa hatua ya fainali ya michuano ya Shirikisho ya Azam itakayo pigwa wikiendi hii huku akiweka nafasi ya tano kwenye msimamo wa ligi.

Loading...
Chanzo: bongo5.com