Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Australian Open 2018: Roger Federer amtupa nje mbabe wa Nadal, atinga fainali kwa kishindo

2027 4898FAF000000578 5315695 Image A 69 1516960290230 TZW

Sun, 28 Jan 2018 Chanzo: bongo5.com

Bingwa wa mchezo wa tenisi duniani Roger Federer amefanikiwa kutinga katika hatua ya fainali ya michuano ya Australian Open 2018.



Federer ambaye anashika namba moja katika viwango vya ubora wa mchezo huo dunian, ametinga katika hatua hiyo baada ya kumtupa nje Chung Hyeon, 21, kwa seti 6-1 5-2.

Mchezo huo ulichezwa kwa muda wa dakika 63 pekee kutokana na Hyeon kupata majeraha ya mguu wake wa kushoto ambapo alishindwa kuendelea na mchezo huo na kuamua kujitoa.

Kutokana na ushindi huo wa Roger Federer atakutana na Marin Cilic kutoka Croatia katika mchezo wa fainali ambao utapigwa Jumapili ya January 28, mwaka huu.



Endapo Federer atafanikiwa kushinda fainali hiyo litakuwa ni taji lake la sita katika mashindano hayo na taji lake la 20 katika mashindano yake yote makubwa tangu alipoanza kucheza mwaka 1998.

Chanzo: bongo5.com