Mon, 26 Feb 2018
Chanzo: bongo5.com
Kocha Msaidizi wa Klabu ya Simba, Masoud Djuma amezungumzia hali ya mlindalango wao Aishi Manula kuwa yupo vizuri na atakuwa sehemu ya wachezaji watakao ingia uwanjani hii leo kuwavaa Gendarmerie mchezo wa kombe la Shirikisho barani Afrika.
Aishi yupo vizuri alipata changamoto hiyo kidogo jana mazoezini ila anaendelea vizuri Watanzania tu watuombee na atacheza mechi.
Timu nzima ipo tayari na wote watakuwepo rabda nahodha wao John Bocco ndo hatakuwepo katika kupambana kwenye mechi ya leo tunawaomba watu watuombee tunajua siyo kazi nyepesi.
Katika mchezo wa kwanza uliyopigwa jijini Dar es Salaam Simba SC ilichomoza na ushindi wa mabao 4 – 0 dhidi ya Gendarmerie .
Chanzo: bongo5.com