Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Asante Kwasi wa Simba aanza mazoezi rasmi kuwavaa Ndanda

675 25023459 154589818507162 4009485595838513152 N TZW

Wed, 27 Dec 2017 Chanzo: bongo5.com

Hatimaye beki kisiki kutoka Lipuli FC, Asante Kwasi ameanza rasmi mazoezi na klabu yake mpya ya Simba SC.

Asante Kwasi akiwa na Mbaraka Yusuph wa Azam FC katika ufukwe wa Coco

Kwasi ambaye usajili wake uliteka vichwa vya habari, ameanza mazoezi na timu yake hiyo mpya leo asubuhi katika fukwe za Coco Beach jijini Dar es Salaam kwa ajili ya mechi za ligi kuu na michuano ya kimataifa.

Simba inadaiwa kulipa kiasi cha shilingi milioni 35 kwa kumsajili beki huyo raia wa Ghana.

Timu hiyo ambayo inaoongoza msimamo wa ligi kuu Tanzania Bara kwa pointi 23, siku ya Jumamosi itashuka uwanjani kupambana na Ndanda FC katika uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara.

Chanzo: bongo5.com