Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Arsene Wenger azungumzia ujio wa Aubameyang

1793 Arsene Wenger TZW

Tue, 23 Jan 2018 Chanzo: bongo5.com

Meneja wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amethibitisha kuendelea kwa mazungumzo ya kumsajili mshambuliaji wa timu ya Borussia Dortmund, Pierre-Emerick Aubameyang.



Aubameyang mshambuliaji huyo wa kimataifa wsa Gabon amehusishwa kujiunga na the Gunners na Wenger amesema kila kitu kinaendelea.



Alipoulizwa na waandishi wa habari kama anauhakika wa kunasa saini ya Aubameyang, Wenger amesema “Kuwe na uhakika kusiwe na uhakika, mi sijui.”

Wenger ameongea “Huwezi jua ni kwa jinsi gani dirisha la usajili litakavyo kamilika.”

“Hivi ni vitu ambavyo uwezekano wa kukamili upo lakini pia tuna mambo mengine tunayofikiria mbali na usajili huo na nafasi tunayo na muda bado haujakwisha.”

“Kwa kipindi hiki bado hatujakamilisha dili lolote kuhusu Aubameyang au mtu mwingine yeyote.”

 Alipoulizwa kama mchezaji wake, Olivier Giroud atakuwa sehemu ya dili la kumnasa Aubameyang kwa yeye kuelekea Dortmund, Wenger amesema kuwa mazungumzo hayajafikia katika hatua hiyo.

Timu hiyo imekamilisha mpango wa Alexis Sanchez kutua Manchester United huku Arsenal ikinufaika kwa kumnasa Henrikh Mkhitaryan.

Chanzo: bongo5.com