Klabu ya Arsenal ya nchini Uingereza imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya michuano ya Europa League baada ya kutoka sare ya 2 – 2 dhidi ya CSKA Moscow kwenye dimba la Arena CSKA na hivyo kusonga mbele kwa jumla ya mabao 6-3.
Kwenye mchezo huo uliyokuwa na ushindani mkubwa, CSKA Moscow ilianza kupata mabao yake kupitia kwa wachezaji wake, F Chalov dakika ya 39 na K Nababkin (50) waka upande wa Arsenal, Danny Welbeck aliipatia bao la kwanza (75) kisha Ramsey akatupia lapili daki ya (90+2) na kujihakikishia kusonga mbele.
Kikosi kamili cha timu zote mbili CSKA Moscow: Akinfeev (6), A. Berezutski (6), Ignashevich (6), V. Berezutski (6), Nababkin (7), Bistrovic (6), Kuchaev (6), Dzagoev (6), Golovin (7), Musa (6), Chalov (7)
Wachezaji waakiba : Vitinho (6), Natkho (6), Milanov (6)
Arsenal: Cech (5), Bellerin (5), Monreal (5), Mustafi (5), Koscielny (5), Elneny (5), Wilshere (5), Ramsey (5), Welbeck (6), Ozil (6), Lacazette (5)
Wachezaji waakiba : Chambers (6), Iwobi (6)
Mchezaji bora wa mchezo huo: Aleksandr Golovin
5 – Arsenal are the fifth English team to reach the semi-finals of the Europa League, after Fulham (2009/10), Liverpool (2009/10 and 2015/16), Chelsea (2012/13) and Man Utd (2016/17). Spread. pic.twitter.com/wEnUPY673z
— OptaJoe (@OptaJoe) April 12, 2018
Arsenal inakuwa miongoni mwa timu tano za Uingereza zilizofanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo ya Europa League baada kufanya hivyo kwa klabu ya Fulham msimu wa mwaka 2009/10, Liverpool msimu wa mwaka 2009/10 and 2015/16 , Chelsea mwaka 2012/13 na Man Utd mwaka 2016/17.
Picha za matukio ya uwanjani kwenye mchezo huo wa Europa League uliyopigwa usiku wa kuamkia leo