Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Arsenal chupuchupu, Wenger atupa lawama kwa muamuzi

1063 47BCC5FD00000578 0 Image A 1 1515019292615 TZW

Thu, 4 Jan 2018 Chanzo: bongo5.com

Klabu ya Arsenal hapo jana imetoka sare ya mabao 2-2 mbele ya Chelsea katika mchezo wa ligi kuu nchini Uingereza maarufu kama London derby.

Meneja Arsene Wenger amemshushia lawama muamuzi wa mchezo huo, Anthony Taylor kwa kuipatia Chelsea penati ambayo anaamini haikustaili na kuifanya timu hiyo kusawazisha bao kupitia kwa Eden Hazard dakika ya 67.

The Gunners ilikuwa ya kwanza kupata bao kupitia kwa mchezaji wake Jack Wilsher dakika ya 63 lakini Eden Hazard akaisawazishia Chelsea dakika nne baadae kisha Marcos Alonso akiandikia The Blues bao la kuongoza dakika ya 84 kisha Hector Bellerin akaibuka shujaa wa mchezo baada ya kuisawazishia Arsenal bao la pili dakika za nyongeza na kuufanya  kumalizika kwa sare ya 2-2.

Mchezaji,  Marcos Alonso akiiandikia The Blues bao la kuongoza dakika ya 84

Kikosi cha Arsenal Cech (7), Holding (6), Mustafi (6), Chambers (5), Bellerin (7), Xhaka (6), Wilshere (7), Maitland-Niles (6), Ozil (8), Sanchez (7), Lacazette (6).

Waliyokuwa benchi: Walcott (5), Welbeck (5).

Chelsea: Courtois (8), Cahill (6), Christensen (6), Azpilicueta (6), Moses (5), Kante (6), Bakayoko (5), Alonso (7), Fabregas (6), Hazard (8), Morata (6).

Waliyokuwa benchi: Drinkwater (5), Zappacosta (6), Willian (5).

Mchezaji bora wa mchezo huo ni Eden Hazard.

Chanzo: bongo5.com