Wed, 28 Mar 2018
Chanzo: bongo5.com
Mchezaji tennis raia wa Uingereza, Andy Murray ameanza rasmi mazoezi katika kituo cha Patrick Mouratoglou academy huko nchini Ufaransa baada ya kupita takribani miezi mitatu tangu kufanyiwa upasuaji.
Bingwa huyo mara tatu wa taji la Grand Slam anatarajia kurejea uwanjani mwezi Juni mwaka huu lakini kunauwezekano mkubwa wa kurudi mapema zaidi ya inavyotarajiwa kufuatia mazoezi makali anayofanya.
Mwanachama mmoja wa kituo hicho ameiyambia AFP kuwa, Andy Murray amewasili usiku wa Ijumaa na kutarajiwa kuwa hapo hadi wiki ya kwanza ya mwezi Aprili.
Chanzo: bongo5.com