KOCHA Mkuu Taifa Stars, Emmanuel Amunike amesema uzoefu mdogo kwa wachezaji wake ndiyo sababu kubwa ya kupokea kipigo cha pili kutoka timu ya taifa ya Kenya 'Harambee Stars'.
Stars jana usiku ilijikuta katika wakati mgumu baada ya kupigwa bao 3-2 na Harambee Stars katika mechi ya Fainali za Afcon zinazofanyika jijini Cairo, Misri.
Amunike amesema kitendo cha timu yake kushindwa kulinda ushindi licha ya kuongoza mara mbili inatokana na uzoefu mdogo.
Amesema matokeo ambayo Stars imeyapata katika mchezo dhidi ya Harambee Stars yanaonyesha kwamba bado kuna safari ndefu ya kujenga wachezaji bora.
Amesema kwasasa kazi kubwa inatakiwa kuanzia kuzalisha vipaji sahihi watakaokuja kuwa wachezaji wenye ubora kwa Taifa Stars wakiungana na wachache wenye uzoefu.
Kocha huyo Mnigeria amesema pia matokeo waliyoyapata sasa yameongeza kitu kwa wachezaji wake ambao wote ni fainali zao za kwanza.
Pia Soma
- Samatta: Tumewaangusha Watanzania
- Taifa Stars, Harambee Stars hainaga ushemeji
- Harambee Stars, Taifa Stars, patachimbika