Thu, 28 Dec 2017
Chanzo: bongo5.com
Kama ungekutana na Prince Harry katika kipindi hiki ungemwambia nini?
Bahati hiyo amekutana nayo bondia Anthony Joshua wiki hii katika kituo cha habari cha BBC Radio 4. Joshua amempongeza Prince Harry kwa kumvalisha pete mpenzi wake Meghan Markle na pia amemtania kwa kumuomba ampatie nafasi ya usaidizi katika ndoa yake.
Bondia huyo amethibitisha hilo kupitia ujumbe alioandika kwenye mtandao wa Instagram unaosomeka, “Back to work this morning! Congrats on everything this year & no pressure on the R4 guest edit!
Chanzo: bongo5.com