Dar es Salaam. Washtakiwa katika kesi ya uhujumu uchumi, Habinder Seth na James Rugamalira wanaendelea kusota rumande takribani miaka miwili, kutokana na upelelezi wa shauri hilo kutokukamilika.
Washtakiwa hao wanaokabiliwa na mashtaka 12.
Wakili wa Takukuru, Leonard Swai amedai leo Juni 20, 2019 mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Kisutu, Huruma Shaidi kuwa shauri limekuja kwa ajili ya kutajwa na kuiomba mahakama ipange tarehe nyingine kutokana na upelelezi kutokamilika.
Baada ya maelezo hayo Hakimu Shaidi ameahirisha kesi hiyo hadi Julai 4,2019 itakapotajwa tena na washtakiwa wamerudishwa rumande.
Katika shtaka la kwanza washtakiwa wanadaiwa kati ya Oktoba 18, 2011 na Machi 19,2014 jijini Dar es Salaam, walikula njama katika nchi za Afrika Kusini, Kenya na India kwa ajili ya kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.
Katika shitàka la pili la kujihusisha na mtandao, washtakiwa hao kati ya Oktoba 18,2011 na Machi 19,2014 jijini Dar es Salaam wakiwa sio watumishi wa umma walitekeleza mtandao huo wa uharibifu kwa lengo la kujipatia faida.
Pia Soma
- Iran yatungua ndege ya Marekani
- Boris Johnson azidi kung’ara kinyang’anyiro cha kumrithi May
- Mbunge CCM asema hali ya uzalishaji wa mazao ya biashara si nzuri