Imebainika kuwa Klabu za England zinalengwa na wadukuzi, ambao wanatuma ankara za ulaghai kuhusu uhamisho wa wachezaji wa nje ya Nchi hiyo.
Suala hilo ni zito, Chama cha Soka Cha England (FA) kimetuma onyo kwa Klabu na kuzitaka kupitia barua pepe zao za usalama na kuzitaka idara zao za fedha kuripoti maombi yoyote wanayoamini ni ya uwongo kwao wenyewe na kwa mamlaka husika.
FA imebainisha kuwa kuna ongezeko la ripoti za barua pepe zilizoigwa au zilizodukuliwa...hasa zinazohusiana na malipo kwa klabu za nje.
Vilabu vimeambiwa kuthibitisha maelezo ya akaunti kabla ya kuagiza FA kufanya malipo na kuangalia mfumo wa FIFA ili kuhakikisha taarifa ni halali.