Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

VIDEO: Samia asema chuki, tamaa za viongozi ziliiponza CCM uchaguzi mkuu 2015

Video Archive
Fri, 14 Feb 2020 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Makamu wa Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amesema CCM kilipata shida kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 kutokana na chuki na tamaa za baadhi ya viongozi wake waliowaengua wagombea wenye sifa, kuwaweka wasiokubalika.

Samia ametoa kauli hiyo leo Alhamisi Februari 13, 2020  jijini Dar es Salaam katika maadhimisho ya miaka 43 ya kuzaliwa kwa chama hicho tawala nchini Tanzania.

Amesema CCM kilijipiga fimbo katika uchaguzi uliopita kutokana na chuki za viongozi na wanachama wake jambo alilodai lilikifanya chama hicho kushindwa katika baadhi ya maeneo.

 

Amewataka kuwa wamoja katika uchaguzi wa mwaka 2020 ili waweze kushinda maeneo mengi zaidi na kuendelea kuongoza Serikali.

Amesisitiza kuwa chama hicho kina hazina ya watu wengi wenye uwezo wa uongozi na kutaka wapewe nafasi wakijitokeza.

Habari zinazohusiana na hii

Advertisement
“Mnakumbuka kilichotokea mwaka 2015, tulipigwa fimbo. Na ile fimbo tulijipiga wenyewe kwa chuki na tama zetu wenyewe. Tuhakikishe fimbo ile isitupige tena kwenye uchaguzi huu,” amesema Samia ambaye pia ni mlezi wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam.

Kiongozi huyo ametoa onyo pia kwa wanachama wa walioanza kujipitisha majimboni kwa lengo la kuwania ubunge katika uchaguzi huo.

Amesisitiza anayefaa kugombea  apewe nafasi ili kukipa chama ushindi badala ya wanachama hao kuenguliwa au kuvuliwa uanachama ili mradi wasipate nafasi kwa sababu tayari viongozi wana watu wao mfukoni.

“Mtu anafaa kugombea lakini anaandikiwa sifa mbovu, kisha anaenguliwa. Mwenendo huu hautupeleki kuzuri, tunapoelekea kwenye uchaguzi mkuu tushikamane ili twende pamoja, tushinde pamoja,” amesema Samia.

 

Chanzo: mwananchi.co.tz