Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, leo Septemba 25, 2021 amewasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, akitokea jijini New York, Marekani alikoshiriki katika Mkutano wa 76 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UN), alikohutubia kwa mara ya kwanza Septemba 23, 2021. Rais Samia amepokelewa na viongozi mbalimbali wa serikali na wa kidini pamoja na wananchi mbalimbali, wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, leo Septemba 25, 2021 amewasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, akitokea jijini New York, Marekani alikoshiriki katika Mkutano wa 76 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UN), alikohutubia kwa mara ya kwanza Septemba 23, 2021. Rais Samia amepokelewa na viongozi mbalimbali wa serikali na wa kidini pamoja na wananchi mbalimbali, wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla.