Aliyekua Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali Prof. Jaffar Mussa Assad amesema kuwa yeye hakumaliza muda wake kazini kama inavyoelezwa, bali aliondolewa kazini kinyume cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
"Nimetambulishwa kama CAG niliyemaliza muda wangu. Hapa unakuja umuhimu wa kuheshimu Katiba. Katiba inasema CAG atastaafu akifikisha miaka 60, au kwa ugonjwa, utovu wa nidhamu, maadili". - Prof Jafari Mussa Assad
"Sipendi kuitwa CAG niliyemaliza muda wangu kwakuwa nilitolewa Ofisini kinyume cha Katiba. Jambo hili linaniudhi sana kwakuwa hatukusimamia Katiba vizuri". - Prof Mussa Assad.