Menu ›
Habari
Wed, 1 Jun 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Aliyekuwa Mkuu Wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya Alfajiri ya leo Jumatano, Juni Mosi, 2022, amefikishwa Moshi mkoani Kilimanjaro akitokea Arusha kwa ajili ya kufunguliwa kesi nyingine mpya.
Sabaya amesafirishwa akitokea Gereza Kuu la Kisongo jijini Arusha kwa kuwa yupo mahabusu kutokana na kukabiliwa na mashtaka mengine ya uhujumu uchumi yasiyokuwa na dhamana.
Ikumbukwe kuwa siku ya jana, Mei 31, 2022 Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha iliahirisha hukumu ya kesi ya Uhujumu uchumi inayomkabili Sabaya na wenzake sita hadi, Juni 10, 2022.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles:
- Dabo awavaa Mastaa Azam FC, awapa onyo hili..!
- Duke Abuya mchezaji Bora wa mwezi Singida Big Stars
- Viongozi wa jeshi Niger waukataa ujumbe wa Ecowas
- Wakili Kibatala, Shahidi wachuana taratibu za kumtambua mtuhumiwa
- BREAKING: Sabaya na wenzake waachiwa huru kesi ya uhujumu uchumi
- Read all related articles