Lifestyle

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

SIL

Dogo scout anavyojifua mazoezi makali, ntoto yake kuwa Mwanajeshi "ipo siku nitatoboa" (+video)

Video Archive
Mon, 23 Nov 2020 Chanzo: millardayo.com

Kutana na Juma Ramadhan Juma Scout kutoka Kigoma Tanzania, amefanya scout kwa miaka mitatu sasa na ndoto yake ni kuwa Mwanajeshi.

“Mungu akiniweka hai nahitaji niwe Mwanajeshi ndio ndoto yangu kubwa, kwa sasa nasoma form III na kuna vitu vingi vinanishawishi mimi kuwa Mwanajeshi” Juma Ramadhan

“Huwa naangalia sana movie za kivita, navutiwa na vita ya uso kwa uso unakuta Wanajeshi wamemaliza silaha wanapambana mkono kwa mkono, hiyo huwa inanivutia sana” Juma Ramadhan

“Mama yangu alinikatalia mwanzoni kujiunga scout kwamba inanipotezea muda nikiwa form one ikabidi nijitoe scout, baadae nilimuelezea kwamba scout inafundisha amani na upendo akaanza kunielewaelewa” Juma Ramadhan

Chanzo: millardayo.com