Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

MenuMichezo
Tennis

Tsitsipas Atinga Fainali ya Monte Carlo Masters

Montee Carloo Masters Tsitsipas Atinga Fainali ya Monte Carlo Masters

Sun, 17 Apr 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Bingwa mtetezi Stefanos Tsitsipas amefanikiwa kutinga fainali ya Monte Carlo Masters, ambapo atavaaana na Mhispania Alejandro Davidovich Fokina.

Tsitsipas mchezaji namba 3 kwa ubora duniani alimuondoa Alexander Zverev kwa seti 6-4 6-2 na kumaliza matumaini ya Mjerumani huyo kumaliza mataji matatu ya mataji 1000 ya ATP Masters 1000 na kumkaribia Daniil Medvedev katika viwango.

“Ilikuwa nzuri,” alisema Tsitsipas katika mahojiano yake uwanjani. “Sijui kama mechi ndefu ilinipa nafasi nzuri, lakini niliweza kucheza tenisi nzuri leo. Nina furaha na kiwango nilichoweza kuonyesha na kuja na mawazo mazuri kwenye uwanja.”

Wakati huo, Davidovich Fokina aliendeleza kiwango chake wa kuvutia baada ya kumuondoa Grigor Dimitrov kwa seti 6-4 6-7 (7-2) 6-3 na kufika fainali yake ya kwanza ya ATP Tour.

Mhispania huyo mwenye umri wa miaka 22 amekuwa katika kiwango bora katika michezo ya wiki hii – ambayo ni pamoja na kumuondoa mchezaji namba 1 Novak Djokovic, bingwa wa Indian Wells Taylor Fritz na mkongwe wa Ubelgiji David Goffin.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live