Serena (40) anatarajia kutoa ujumbe wa kuaga mashabiki wake na mashabiki wa mchezo wa Tenis.
Mshindi huyo mara 23 wa michuano mikubwa ya tenis huenda ndo ikawa mara ya mwisho kuonekana katika michuano hiyo mikubwa.
Katika mchezo wake wa mwisho Williams alichapwa 6-4, 6-0 na Muingereza Emma Raducanu ambaye mwenyewe alitolewa nje ya Australian Open na Kovinic mnamo Januari.
Siku ya Jumamosi, waandaaji wa michuano hiyo walithibitisha kwamba yeye na dada yake mkubwa Venus Williams walikuwa wamepewa kadi ya pori katika mashindano ya wanawake wawili wawili, ambayo yataanza Jumatano.
“Nadhani yeye ndiye kitu kikubwa zaidi kitakachowahi kuwa kwenye mchezo huu,” Naomi Osaka wa Japan alisema Jumamosi.
Serena amecheza kwa mafanikio Zaidi mchezo huo hivyo anatarjiwa kuacha alama itakayokumbukwa na wapenda mchezo huo wa Tenis.