Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

MenuMichezo
Tennis

Naomi Osaka Kutoshiriki Mashindandano ya Wimbledon

Naomi Osaka 1 Naomi Osaka

Mon, 20 Jun 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mcheza tennis anayeshika namba moja kwa ubora duniani Naomi Osaka hataweza kushiriki mashindano ya Wimbledon kutokana na majeraha aliyoyapata akiwa anashiriki michuano ya Madrid Open na sababu ya kutopanda kwa viwango mwaka huu kwenye mashindano hayo.

Naomi Osaka majeraha aliyoyapata kwenye michuano ya Madrid Open yalimfanya akose mashindano ya WTA 1000 jijini Rome, pia ilipelekea kutolewa kwenye mashindano ya French Open, ambapo alipoteza dhidi ya mpinzani wake Amanda Anisimova kwenye mzunguko wa kwanza.

Naomi Osaka mshindi wa Grand Slam nne, alieleza hisia zake na sababu ya kutoshiriki kwenye mashindano ya Wimbledon, ukiondoa majeraha aliyoyapata kwenye mashindano ya Madrid Open.

“Majeraha yangu ya ankle ya ndani bado hayajapona, tutaonana mashindano mengine,” aliandika kwenya ukurasa wake wa Twitter

“Nahisi kucheza mashindano ya Wimbledon ni kama maonyesho zaidi. Najua hii si kweli, sawa, lakini akili yangu inahisi hivyo.

“Ningependa nishiriki, ili kupata uzoefu kwenye uwanja wa majani, lakini muda huo huo ningependa kupata hamasa nikiona napanda viwango zaidi.” Alisema Naomi Osaka.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live