Sat, 22 Jan 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mchezaji namba 2 kwa ubora duniani (wanaume), Daniil Medvedev, amefuzu hatua ya 16 bora kunako mashindano ya Australian Open.
Medvedev alikua uwanjani akichuana na Botic van de Zandschulp katika uwanja wa Margaret Court Arena. Daniil anaingia kwenye mashindano haya akiwa na kumbukumbu ya kucheza fainali mwaka jana na pia, ni bingwa mtetezi wa US Open mwaka huu.
Ushindi wa seti 6-4 6-4 6-2, unamvusha Daniil kwenye hatua ya 4 na sasa, atachuana na mshindi kati ya Christopher O’Connell au Maxime Cressy.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live