Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

MenuMichezo
Tennis

Caroline Garcia afuzu nusu fainali US Open

Caroline.png Caroline Garcia ameshinda michezo 13 mfululizo

Wed, 7 Sep 2022 Chanzo: eatv.tv

Mcheza tennis raia wa Ufaransa Caroline Garcia amefuzu kwa mara ya kwanza kucheza hatua ya nusu fainali kwenye tennis. Hii ni mara baada ya kumfunga Coco Gauff raia wa Marekani kwenye mchezo wa robo fainali ya michuano ya wazi ya Marekani (US Open).

Carolina amemfunga Gauff kwa seti mbili mfululizo 6-3 na 6-4 kwenye mchezo uliochezwa katika dimba la Arthur Ashe. Raia huyo wa ufaransa ambaye anashika nafasi ya 17 kwenye viwango vya ubora kwa wanawake amekuwa kwenye kiwango bora kwani huu ni mchezo wake wa 13 mfululizo ameshinda.

Na katika hatua hiyo ya nusu fainali atacheza dhidi ya mtunisia Ons Jabeur ambaye amefuzu kucheza katika hatua hiyo baada ya kumfunga Ajla Tomlijanovic na kuweka rekodi yakuwa mwanamke wa kwanza kutoka Afrika kufuzu hatua ya nusu fainali.

Chanzo: eatv.tv