Kinda wa Tenisi, Carlos Alcaraz alimaliza wiki kwa kutwaa Ubingwa kwa ushindi wa seti moja kwa moja dhidi ya Alexander Zverev katika fainali ya Madrid Open.
Baada ya ushindi dhidi ya Role Model wake Rafael Nadal katika robo-fainali na Novak Djokovic aliyeshika nafasi ya juu katika nusu-fainali, chipukizi huyo wa Uhispania alifanikiwa kupata ushindi dhidi ya Zverev kwa seti 6-3, 6-1.
Alcaraz, ambaye alishinda taji lake la kwanza la Masters 1000 mjini Miami mwezi uliopita, alifanikiwa kupata ushindi dhidi ya mchezaji namba 3 kwa ubora duniani na kutwaa taji lake la pili akiwa na miaka 19 tu.
Alcaraz aliorodheshwa namba 120 kwa ubora duniani mwaka mmoja uliopita, lakini sasa atapanda hadi namba 6 kwa ubora katika viwango vipya siku ya leo [Jumatatu].
Zverev alikuwa akijaribu kushinda taji lake la pili mfululizo la Madrid Open na la tatu kwa jumla, baada ya ushindi wake wa mwaka 2018 kwa kumshinda Matteo Berrettini katika fainali ya mwaka jana.