Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

MenuMichezo
Tennis

Belinda Bencic Bingwa wa Charleston Open

Belinda Bencic Belinda Bencic

Mon, 11 Apr 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mshindi wa Tenisi wa michuano ya Olimpiki, Belinda Bencic amefanikiwa kutwaa taji la Charleston Open baada ya kumfunga Ons Jabeur katika seti tatu kwa upande wa wanawake.

Mswisi huyo mwenye umri wa miaka 25 alitwaa taji hilo upande wa WTA kwa kumshindwa Mtunisia Jabeur kwa seti 6-1, 5-7, na 6-4 katika pambano lililodumu kwa saa 1 na dakika 35.

Belinda ambaye ni mchezaji namba 4 wa zamani wa dunia kwa ubora alimfunga Marketa Vondrousova na kutwaa Olympic Gold mjini Tokyo katika majira ya kiangazi yaliyopita na kushinda taji lake la 6 la WTA na kupanda mpaka nafasi ya 13 kutoka nafasi ya 21.

Mchezaji namba 10 kwa ubora duniani Jabeur alidhibitiwa vikali katika koti ya wazi na kupoteza mchezo wake wa kwanza wa kujitolea kwa mara ya pili.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live