Yametimia, baada ya miaka 44, Ashleigh Barty anakuwa raia wa kwanza wa Australia kutwaa ubingwa wa Australian Open.
Barty ameibuka kidedea baada ya kumfunga Danielle Collins kwa matokeo ya seti 6-3 7-6 7-2 ukiwa ni mchezo ambao ulitawaliwa na upinzani mkubwa.
Ashleigh Barty alianza kwa kuongoza kwenye seti ya kwanza kabla ya Collins kuonesha maajabu yake kwenye seti ya pili kwa kuongoza 4-0. Kuelekea mwishoni mwa seti ya 2, Barty alionesha ubora na uhodari wake uwanjani kwa kushambulia na kusawazisha matokeo kuwa 4-4.
Piga n’kupige ziliendelea kwenye seti ya pili mpaka matokeo kuwa 7-6 na mchezo kuamuliwa kwa tie break na champion set ambazo, Barty alishinda kwa matokeo ya 7-2.
Ushindi wa Barty unakuwa ni ushindi wake wa 3 wa Grand Slams huku Collins akiwa kwenye nafasi kubwa ya kuingia kwenye orodha ya wachezaji 10 bora duniani (kwa wanawake) mwaka huu.