Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

MenuMichezo
Tennis

Andrey Rublev Bingwa Serbian Open

MMMM Andrey Rublev Bingwa Serbian Open

Tue, 26 Apr 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mcheza Tenisi wa Urusi, Andrey Rublev amefanikiwa kutwaa ubingwa wa Serbian Open baada ya kumfunga mchezaji namba moja kwa ubora duniani, Novak Djokovic katika fainali mjini Belgrade.

Djokovic alicheza kwa mara ya nne wiki hii mbele ya mashabiki wake wa nyumbani mjini Belgrade, lakini alishindwa katika fainali dhidi ya Rublev aliyeibuka na ushindi wa 6-2 6-7 (4-7) 6-0 katika mchezo uliodumu kwa saa mbili na dakika 29.

Ulikuwa ushindi wa kwanza wa Rublev, 24 dhidi ya mchezaji namba moja duniani na kumpa mchezaji huyo taji la tatu la tour-level msimu huu na kufikia rekodi ya Rafael Nadal katika ushindi wa kwanza huko Marseille na Dubai mnamo Februari.

Djokovic alikosa sehemu kubwa ya mashindano msimu huu, ikiwemo mashindano ya Australian Open na ATP Masters 1000 huko Miami na Indian Wells, kwa sababu ya kukataa kupata chanjo dhidi ya Covid-19 kabla ya kurejea na kupoteza katika mchezo wa mapema katika mashindano ya Monte Carlo Master.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live