Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Aziz Ki: Fei Toto atabaki kuwa ndugu yangu

Aziz  Ki Yanga Ml Aziz Ki

Wed, 15 May 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Kiungo mshambuliaji wa Klabu ya Yanga, Stephanie Azizi Ki ameesema kuwa kungo wa Azam FC, feisal Salum Abdallah 'Fei Toto' atabaki kuwa ndugu yake na kwamba malengo yake yalikuwa kuisaidia timu kupata ubingwa na sio kujifikiria yeye kuhusu ufungaji bora.

Aziz ambaye alisajiliwa na Yanga akitokea ASEC Mimosas mwanzoni mwa msimu uliopita amesema hayo baada ya Yanga kutwaa ubingwa juzi mara ya 30 huku ikiwa ni mara ya pili kwa Aziz Ki kutwaa ubingwa huo akiwa na Yanga.

Fei Toto na Aziz Ki wote wanawania kiatu cha ufungaji bora wakiwa wamefunga mabao 15 kila mmoja huku ikiwa imesalia michezo mitatu tu kutamatika kwa Ligi.

Aziz amesema hayo wakati akijibu komenti ya shabiki wake aliyenadika kwenye mtandao wa Instagram kwa maneno kuwa kuwa; "Na hautafunga Milele Mpaka Feisal anachukua kiatu."

Aziz alijibu; "Nishakuwa Bingwa kipaumbele changu kilikuwa kushinda na timu sio mimi peke yangu bali ni timu yote, Feisal atabaki kuwa kaka Yangu, mimi sasa ni bingwa nahitaji kufikiria kuhusu kuwa mfungaji bora."

Chanzo: www.tanzaniaweb.live