Wed, 26 Jun 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Jeshi la Polisi mkoani Simiyu limeanza kutembelea kaya mbalimbali na kubaini zenye watoto wenye ualbino ili kuimarisha ulinzi pamoja na kutoa elimu kwa wazazi na walezi juu ya namna bora ya kuwalinda watoto hao.
Mkaguzi wa polisi kata ya Dutwa, Canatus Kamihanda amesema anafanya zoezi hilo kwa kushirikiana na polisi jamii pamoja na wenyeviti wa vijiji na vitongoji.
Dutwa aliyeanza kufanya zoezi hilo katika kata yake, amewasisitiza wazazi na walezi kuwalinda watoto hao na kutoa taarifa pale wanapoona kuna viashiria vya hatari.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live