Mwanaume mmoja aliyefahamika kwa jina Nyili Katerezi (40) Mkazi kitongoji cha Kanywengezi kijiji cha Nyandago kata ya Butundwe Wilayani Geita, amefariki baada ya kujeruhiwa vibaya na Mnyama aina ya Kiboko wakati akiwa kwenye majukumu ya uvuvi katika mwalo wa Nyandago majira ya saa kumi usiku.
Mwanaume mmoja aliyefahamika kwa jina Nyili Katerezi (40) Mkazi kitongoji cha Kanywengezi kijiji cha Nyandago kata ya Butundwe Wilayani Geita, amefariki baada ya kujeruhiwa vibaya na Mnyama aina ya Kiboko wakati akiwa kwenye majukumu ya uvuvi katika mwalo wa Nyandago majira ya saa kumi usiku. Akizungumza kwa niaba ya familia Martin Mlengosha amesema wamepokea kwa masikitiko makubwa tukio la kujeruhiwa kwa Mtoto wao na mnyama aina kiboko na kupelekea kupoteza maisha.