Tue, 4 Jun 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Kanda ya Nyasa Mchungaji Peter Msigwa amesema kuwa ataendelea kusalia CHADEMA na hana mpango wa kuhama.
Msigwa ameyasema hayo June 3, 2024 wakati akizungumza na Waandishi wa Habari na Wanachama wa CHADEMA Manispaa ya Iringa.
“Najua wabaya wangu wengi walikuwa wanatoa ramli labda mimi leo nitahama siondoki siendi popote nipo CHADEMA sihami CHADEMA tutapambana humu humu yule anayetaka kunyofowa wengine atanyofolewa yeye tunachotaka haki itendeke hatutoogopa cheo cha Mtu wala sura ya mtu.”
Chanzo: www.tanzaniaweb.live