Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, ametahadharisha kuhusu matumizi ya fedha za umma, akiitaka serikali ibane matumizi.
Mbowe ametoa tahadhari hiyo kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii leo Juni 27, 2024; akionya kwamba nchi haiwezi kuendelea ikiwa asilimia 89 ya pato la nchi itatumika kulipa madeni na kuendesha serikali.
"Kama nchi, tunalipa wakati huo huo tunaendelea kukopa mikopo mikubwa. Serikali ya CCM haioni umuhimu wa kupunguza matumizi ili kuelekeza sehemu kubwa zaidi ya bajeti kuletea Watanzania maendeleo; tuwapumzishe," amesema.
"Katika pato la taifa kwa mwaka tunatafuna asilimia 89 kwa mambo mawili; madeni (asilimia 51) na matumizi ya serikali (asilimia 38). Pesa kidogo iliyobaki haikidhi kuendesha miradi ya maendeleo katika nchi hii."