Tue, 17 Sep 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Taifa, Freeman Mbowe na Makamu Mwenyekiti Bara, Tundu Lissu wakiwasili makao makuu ya chama hicho, Mikocheni jijini Dar es Salaam leo Jumanne Septemba 17, 2024.
Miongoni mwa mambo yatakayojadiliwa kwenye kikao cha Kamati Kuu Chadema cha Septemba 17 hadi 18, 2024 ni hali ya usalama wa nchi.
Kikao hicho pia, kinatarajia kufanya usaili na kuteua wagombea wa nafasi mbalimbali za uongozi katika kanda za Pwani, Kusini na Pemba.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live