Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA - Bara, Tundu Lissu amsema endapo CHADEMA itaacha misingi yake iliyomfanya ajiunge nacho basi ataondoka katika chama hicho kwakuwa si dhambi na CHADEMA si Dini na si mama yake
Akizungumza kupitia Mtandao wa Club house amemnukuu Mwalimu Nyerere aliyewahi kusema CCM siyo mama yake na ikiacha misingi yake ataiacha, na kuongeza kuwa “Unataka niseme kwa mazingira yoyote yale vyovyote itakavyokuwa sitahama CHADEMA? ni mama yangu?”
Ameongeza “Nitakuwa sina sababu ya kubaki na hiyo siyo dhambi. Ni Chama cha Siasa, Vyama vya Siasa huja na kuondoka, sisi binadamu tunakuja na kuondoka, kwa hiyo usiniombe nijifunge minyoro ya aina hiyo”.