Alyekuwa mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema amezidi kukazia kauli yake kuwa bodaboda sio kazi salama kwa vijana.
Lema amesema, yupo tayari kupoteza hata ubunge kama endapo hawatamchagua kwa kuwaeleza ukweli huo kwani yeye mshahara wa ubunge kwake sio kitu na anaweza kuwalipa wabunge wanne mshahara na akawapa kazi ya kumtetea mke wake.
"Siishi kwa ajili ya kuwa mbunge, naishi kwa ajili ya baraka ya kizazi kinachokuja. Ubunge, mimi ni mchaga, sipigani kuwa mbunge ili nipate mshahara wa milioni kumi, mshahara wa milioni kumi ni kidogo sana.
"Naweza kuwalipa wabunge wanne kila mwezi na nikawapa kazi moja tu ya kumtetea mke wangu pindi ninapochelewa kurudi nyumbani," alisema Lema.
"kama kuwambia ukweli Bodaboda itanifanya nikose ubunge nipo tayari" Mh. @godbless_lema pic.twitter.com/NvzB7NJOnI
— Twaha Mwaipaya (@Twaha_Mwaipaya) March 6, 2023