Mon, 2 Sep 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kamati Kuu Maalumu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), chini ya uenyekiti wa Rais Samia Suluhu Hassan iliyokutana leo Jumapili, Septemba 1, 2024 pamoja na mambo mengine imewavua madaraka viongozi wake wawili akiwemo wa Jumuiya ya Wanawake (UWT).
Chama hicho kimemuondoa Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Lindi, Palina Ninje pamoja na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Bagamoyo, Abdul Zahoro.
Uamuzi huo umetangazwa na Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM, Amos Makalla wakati akizungumza na waandishi wa habari akitoa mrejesho wa yaliyozungumzwa kwenye kikao cha kamati hiyo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live