Tue, 16 Jul 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Chama Cha Mapinduzi kupitia Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Itikadi, Uenezi na Mafunzo Ndg. Amos Makalla kimemjibu Mbunge wa Mtama Ndg. Nape Nnauye kuhusu imani yake juu ya ushindi katika chaguzi mbalimbali nchini.
Makalla amesisitiza kuwa CCM haihitaji mbeleko na itashinda kutokana na rekodi nzuri ya kuwaletea wananchi maendeleo. Aidha, amesisitiza kuwa kauli iliyotolewa na kiongozi huyo haikihusu Chama Cha Mapinduzi na ni mawazo yake yeye mwenyewe.
CCM itaendelea kuheshimu demokrasia na maamuzi yeyote ya wananchi kupitia sanduku la kura kama ilivyo siku zote.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live