Wed, 27 Jul 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Wachezaji saba wa timu ya taifa ya Rugby ya nchini Australia wameamua kugomea mechi muhimu kutokana na timu yao kuamua timu ivae jezi zinazohamasisha mahusiano ya jinsia moja.
Wachezaji hao wamesema kuwa hawakuulizwa maoni yao juu ya jezi hizo ambazo ziko kinyume na maadili yao ya kidini na kitamaduni.
Klabu hiyo imeomba msamaha kwa suala hilo huku kocha akikiri kuwa uongozi wa klabu umefanya "kosa kubwa".
Kwa sheria za ligi wachezaji wa timu moja hawawezi kuvaa jezi tofauti hivyo ufumbuzi unahitajika kabla ya mechi hiyo ambayo imepangwa kuchezwa Alhamisi wiki hii.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live