Miongoni mwa habari kubwa za wiki hii kwenye tasnia ya michezo Ulimwenguni ni ile inayomhusu mwanariadha maarufu kutoka Jamaica, Usain Bolt anayetajwa kuwa Binadamu mwenye kasi zaidi katika historia, ametuma maombi ya kupata hakimiliki ya pozi lake ambalo amekua akilionesha kila anaposhinda.
Usain aliwasilisha maombi yake hayo katika Ofisi za alama ya Biashara nchini Marekani (the U.S. Patent and Trademark Office).
Bolt anapanga kutumia picha hiyo kama nembo kwenye bidhaa zitakazojumuisha nguo, miwani ya jua, vito vya thamani, mifuko, migahawa na pia katika duka atakalofungua kwaajili ya kuuza bidhaa hizo.