Wed, 31 May 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mavis Paterson, Bibi mwenye umri wa miaka 85 amekamilisha safari ya maili 1,000 (takribani kilomita 1610) kwa kutumia Baiskeli na kufanikiwa kuchangisha pauni elfu 60 za misaada.
Bibi huyo alifanya safari hiyo ndefu akizunguka nchini Scotland kwa ajili ya kumbukumbu ya watoto wake watatu waliofariki kwa magonjwa mbalimbali kati ya mwaka 2012 na 2016.
Aliianza safari hiyo mwishoni mwa mwezi Aprili na kuikamilisha Jumapili ya juzi alipopokelewa kwa shangwe na umati wa watu.
Pesa alizochangisha zitakwenda kwenye taasisi moja inayojihusisha na kusaidia wagonjwa wa saratani.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live