Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Vipimo vipya vya damu 'vyaweza kutabiri' kurejea tena kwa saratani ya matiti

Vipimo Vipya Vya Damu 'vyaweza Kutabiri' Kurejea Tena Kwa Saratani Ya Matiti Vipimo vipya vya damu 'vyaweza kutabiri' kurejea tena kwa saratani ya matiti

Mon, 3 Jun 2024 Chanzo: Bbc

Vipimo vipya vya damu vya "kina zaidi" vyaweza kutabiri ikiwa saratani ya matiti itarejea miaka kadhaa kabla ya ugonjwa huo kuonekana kwenye vipimo vya uchunguzi, watafiti wanasema.

Ilichukua sampuli za DNA ya uvimbe kabla ya kurudi tena na ilipatikana kuwa sahihi 100% katika kutabiri ni wagonjwa gani saratani yao itarejea.

Inatarajiwa kuwa kipimo kinaweza kuruhusu matibabu kuanza mapema na kuimarisha viwango vya kuishi.

Utafiti wa Uingereza umetajwa kuwa "wa kipekee" na wataalam lakini bado uko katika hatua zake za awali.

Saratani ya matiti ni aina ya kawaida ya ugonjwa huo ulimwenguni, ambapo wanawake milioni 2.26 waligunduliwa mnamo 2020 na vifo 685,000 vikatokea katika mwaka huo huo, kulingana na shirika la saratani ya matiti Uingereza.

Timu ya watafiti kutoka Taasisi ya Utafiti wa Saratani (ICR) London ilifanya majaribio kwa wagonjwa 78 wenye aina tofauti za saratani ya matiti katika hatua ya awali.

Kwa wastani, kipimo cha damu kiligundua saratani miezi 15 kabla ya dalili kuonekana au ugonjwa kuonyeshwa kwenye vipimo, kulingana na matokeo yaliyowasilishwa kwenye mkutano wa Jumuiya ya Kitabibu huko Chicago Jumapili.

Ugunduzi wa mapema zaidi ulikuwa miezi 41 kabla ya uchunguzi kuthibitisha utambuzi.

Mtafiti mkuu Dk Isaac Garcia-Murillas, kutoka ICR, alisema: "Seli za saratani ya matiti zinaweza kubaki mwilini baada ya upasuaji na matibabu mengine lakini kunaweza kuwa na seli chache sana ambazo hazionekani kwenye uchunguzi wa ufuatiliaji."

Aliongeza kuwa seli hizo zinaweza kusababisha mgonjwa kuanza kudhoofika tena miaka mingi baada ya matibabu yao ya awali.

Dk Garcia-Murillas alisema utafiti huo unaweka msingi wa ufuatiliaji bora wa baada ya matibabu na matibabu yanayoweza kuongeza siku za kuishi.

Watafiti walijaribu sampuli za damu wakati wa utambuzi, kisha ikafuatia upasuaji na matibabu ya kemikali yaani chemotherapy.

Chanzo: Bbc