Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Serikali yashusha gharama za kusafisha figo

Wizara Afyatz Mollel Serikali yashusha gharama za kusafisha figo

Tue, 27 Aug 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Serikali kupitia Bohari ya Dawa (MSD) inafanya jitihada za kununua vitendanishi na vifaa vinavyotumika kusafisha figo moja kwa moja kutoka Viwandani ili kupunguza gharama za huduma hiyo.

Hayo yamesemwa leo Agosti 27, 2024 na Naibu Waziri wa Afya Dkt Godwin Mollel kwa niaba ya Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama wakati wa kipindi cha maswali na majibu bungeni jijini Dodoma.

Aidha Dkt. Mollel amesema serikali imeanza kuchukua hatua katika kupunguza gharama za matibabu kwani kwa Hospitali ya Temeke gharama zimeshuka hadi laki moja na nusu.

Pia, Dkt Mollel ametoa rai kwa wananchi mara utekelezaji wa Bima ya Afya kwa Wote utakapoanza waweze kujiunga kwani ni njia pekee ya kuweza kuwasaidia kuepuka gharama za matibabu.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live