Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

'Morning Sickness' ipo hivi....

Morning Sickness 'Morning Sickness' ipo hivi....

Fri, 13 Sep 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Katika maisha ya kila siku kwa upande wa kinamama katika huduma za afya ni kawaida kuwahi kukutana na neno la kingereza ‘morning sickness’ kwa Kiswahili ugonjwa wa asubuhi.

Ni hali ambayo huwa ni kawaida kuwapata kinamama wajawazito wakati mimba iliyotungwa ikiwa change, yaani kwenye muhula wa kwanza katika wiki ya sita tangu mimba kutungwa.

Ugonjwa wa asubuhi ni hali ya kuhisi kama kutapika au kichefuchefu au kujisikia hovyo hovyo mara baada ya kuamka. Hali hii hutokana na mabadiliko yanayotokea mara tu mimba inapotungwa.

Pamoja na kuitwa hivyo lakini dalili zake zinaweza kuathiri wakati wowote wa siku au usiku au kujisikia mgonjwa mchana kutwa. Ni hali isiyofurahisha inayoweza kuathiri maisha ya kila siku.

Kwa kawaida hali hii huwa hovyo zaidi katika wiki ya tisa na huisha katika wiki ya 16 hadi 20 ya mimba, ni tatizo ambalo halimweki mtoto aliye katika nyumba ya uzazi katika hatari yoyote ya kiafya.

Ingawa hali hii inaweza kuwa mbaya na kuleta aina ya ugonjwa wa ujauzito inayoitwa ‘hyperemesis gravidarum’ inayoweza kusababisha upungufu wa maji mwilini au kutopata virutubishi vya kutosha kutoka kwa lishe.

Hii ikitokea inahitaji matibabu ya kitaalam, wakati mwingine mjamzito anahitajika kulazwa katika huduma za afya.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live