Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

MenuMichezo
Golf

Wacheza Gofu wamlilia Magufuli

Gofu Pic Data Wacheza Gofu wamlilia Magufuli

Mon, 22 Mar 2021 Chanzo: www.mwanaspoti.co.tz

Kifo cha Rais wa  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ,Hayati John Pombe Magufuli kimeonekana kuwagusa  wachezaji wa gofu ambao wengi walionekana kuwa na  mategemeo  makubwa kuwa angeweza kuusimamia mchezo huo uzidi kukua hapa nchini  na hata katika bara la Afrika.  Katibu mkuu wa Chama cha Gofu cha Wanawake Tanzania, Madina Iddi  Amesema wakati wa utawala wa rais Magufuli mchezo huo ulikuwa na mafanikio makubwa ikiwemo Tanzania  kutwaa ubingwa wa Afrika Mashariki na Kati mwaka  2019 katika mashindano yaliyofanyika Uganda. Madina amesema "Pia katika mashindano ya  kuwania ubingwa wa Afrika yaliyofanyika  nchini Ghana  mwaka 2018 Tanzani tuliweza kushika nafasi ya pili tukiwakilishwa na wachezaji  wanne  nikiwemo mimi,Hawa Wanyeche, Angel Eaton na Neema  Olomi. Mchezaji  huyo alisema wamesikitishwa na msiba huo kwani matamanio yao ya kukutana na rais Magufuli hayajaweza kufanikiwa baada ya mauti kumkuta.    "Tulipanga tuonane naye baada ya kushika nafasi ya pili  katika mashindnao ya kuwania ubingwa wa Afrika   mwaka 2018 na hata tulipotwaa ubingwa wa Afrika Mashariki na kati 2019 bado tulikuwa na ndoto hiyo ya kukutana naye ili kumueleza changamoto zetu. Alisema kifo cha rais Magufuli ni pengo kubwa sana kwani aliweza kuwasaidia kwenda kwenye mashindano ya Afrika kupitia kwa viongozi  aliowachagua wakati huo wa TANAPA. “Kwa hili pia tunamshukuru  sana kwani viongozi aliowateua kipindi kile mwaka 2018 walitusaidia sana kufanikisha safari yetu ya kwenda Ghana, "amesema Madina. Judith Ally ambaye ni mchezaji wa gofu wa timu ya wanawake  ya klabu ya Dar es Salaam Gymkhana amesema kwa upande wake atamkumbuka  rais Magufuli kutokana alivyokuwa na tabia ya kutobagua michezo. "Kwa kweli alikuwa anafuatilia michezo yote na hata ukiwa  kiongozi ndani ya  chama  huwezi kumdanganya kitu ,"anasema  Judith Naye Saidi Ally mchezaji wa gofu wa kulipwa, amesema wamepata pigo kubwa kutokana na jinsi rais Magufuli alivyokuwa mfuatiliaji wa vitu na kujua matatizo ya kila mchezo. "Itachukuwa mda mrefu kuziba pengo lake  kwani ni  rais aliyeonekana kuwa  mfuatiliaji wa kila eneo inasikitisha tumempoteza  kiongozi mahiri,” anasema Ally.

Kifo cha Rais wa  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ,Hayati John Pombe Magufuli kimeonekana kuwagusa  wachezaji wa gofu ambao wengi walionekana kuwa na  mategemeo  makubwa kuwa angeweza kuusimamia mchezo huo uzidi kukua hapa nchini  na hata katika bara la Afrika.  Katibu mkuu wa Chama cha Gofu cha Wanawake Tanzania, Madina Iddi  Amesema wakati wa utawala wa rais Magufuli mchezo huo ulikuwa na mafanikio makubwa ikiwemo Tanzania  kutwaa ubingwa wa Afrika Mashariki na Kati mwaka  2019 katika mashindano yaliyofanyika Uganda. Madina amesema "Pia katika mashindano ya  kuwania ubingwa wa Afrika yaliyofanyika  nchini Ghana  mwaka 2018 Tanzani tuliweza kushika nafasi ya pili tukiwakilishwa na wachezaji  wanne  nikiwemo mimi,Hawa Wanyeche, Angel Eaton na Neema  Olomi. Mchezaji  huyo alisema wamesikitishwa na msiba huo kwani matamanio yao ya kukutana na rais Magufuli hayajaweza kufanikiwa baada ya mauti kumkuta.    "Tulipanga tuonane naye baada ya kushika nafasi ya pili  katika mashindnao ya kuwania ubingwa wa Afrika   mwaka 2018 na hata tulipotwaa ubingwa wa Afrika Mashariki na kati 2019 bado tulikuwa na ndoto hiyo ya kukutana naye ili kumueleza changamoto zetu. Alisema kifo cha rais Magufuli ni pengo kubwa sana kwani aliweza kuwasaidia kwenda kwenye mashindano ya Afrika kupitia kwa viongozi  aliowachagua wakati huo wa TANAPA. “Kwa hili pia tunamshukuru  sana kwani viongozi aliowateua kipindi kile mwaka 2018 walitusaidia sana kufanikisha safari yetu ya kwenda Ghana, "amesema Madina. Judith Ally ambaye ni mchezaji wa gofu wa timu ya wanawake  ya klabu ya Dar es Salaam Gymkhana amesema kwa upande wake atamkumbuka  rais Magufuli kutokana alivyokuwa na tabia ya kutobagua michezo. "Kwa kweli alikuwa anafuatilia michezo yote na hata ukiwa  kiongozi ndani ya  chama  huwezi kumdanganya kitu ,"anasema  Judith Naye Saidi Ally mchezaji wa gofu wa kulipwa, amesema wamepata pigo kubwa kutokana na jinsi rais Magufuli alivyokuwa mfuatiliaji wa vitu na kujua matatizo ya kila mchezo. "Itachukuwa mda mrefu kuziba pengo lake  kwani ni  rais aliyeonekana kuwa  mfuatiliaji wa kila eneo inasikitisha tumempoteza  kiongozi mahiri,” anasema Ally.

Chanzo: www.mwanaspoti.co.tz