Kijamii

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Lifestyle

SIL

MenuKijamiiMaoni
Articles

Viongozi wamkumbuka Karume, mwanaye aeleza alivyopigania muungano

101665 Karume+pic Viongozi wamkumbuka Karume, mwanaye aeleza alivyopigania muungano

Wed, 8 Apr 2020 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Viongozi mbalimbali wamefanya dua katika  kaburi la Rais wa kwanza wa Zanzibar, Abeid Amani Karume katika kumbukumbu ya miaka  48 ya kifo chake.

Rais wa Zanzibar, Ali Mohamed Shein; Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Rais Mstaafu wa Zanzibar,  Amani Abeid Karume ni kati ya waliohudhuria dua hiyo.

Dua hilo limesomwa leo Jumanne Aprili 7, 2020 katika kaburi la kiongozi huyo.

Abeid Amani Karume alizaliwa Agosti 4, 1905  na kufariki Aprili 7, 1972 katika kitongoji cha Pongwe Wilaya ya Magharibi A,  Kisiwani Zanzibar.

Mwanaye,  Balozi Ali Abeid Karume amesema baba yake alikubali muungano kwa sababu alijua Afrika ni kitu kimoja.

 “Asingekuwa Abeid Amani Karume huu muungano wetu Tanzania usingekuwepo na huo ndio ukweli wenyewe kwa sababu hii nchi ilikuwa inatawaliwa na Sultani.”

Pia Soma

Advertisement
 “Kuunganisha nchi sio jambo rahisi, namkumbuka sana huyu mzee kwa sababu alikuwa na moyo wa kujitolea. Kuna nchi nyingi zinashindwa kuungana kwa sababu viongozi wana tamaa,” amesema.

 

Columnist: mwananchi.co.tz