Kijamii

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Lifestyle

SIL

MenuKijamiiMaoni
Articles

UCHOKOZI WA EDO: Wabunge walipogeuka Jose Mourinho Cairo

64463 Edo+kumwembe

Thu, 27 Jun 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Wabunge wetu bwana! Wako fasta kwelikweli. Kama wanapoambiwa wapitishe miswada ambayo bado haijaeleweka halafu msimamo wa chama ukawa ni kupitisha. Wanapitisha fasta. Nawakubali sana.

Majuzi walikuwa Cairo, Misri. Timu yetu ya taifa ipo kule ikicheza katika michuano ya mataifa ya Afrika. wabunge wakaona hakuna namna ya kupata ‘kiki’ ya haraka haraka zaidi ya kwenda Cairo kuwasapoti vijana. Miaka minne sasa tangu utawala wa Namba Moja ulipoingia madarakani, kuna wabunge hawajavuka hata Namanga au Tunduma. Hii ilikuwa fursa.

Tukafungwa mabao 2-0 na Senegal. Mechi ilipomalizika walirudi na kufanya mkutano na waandishi wa habari pale Airport. Walishutumu mengi na hasa kumshutumu kocha, Emmanuel Amunike. Kwa siku za karibuni ni rahisi kusikilizwa kama ukimlaumu kocha wa Taifa Stars kwa kila kitu.

Hata hivyo, sio wote wana ‘moral authority’ (uhalali) wa kumlaumu kocha. Baadhi ya hawa wanaolaumu ndio wanaopitisha bejeti ndogo zaidi ya michezo pale Dodoma. Ni hao hao ambao wameruhusu tuwe na viwanja vibovu zaidi katika ligi kuu yetu. Viwanja vingi ni vya chama chao.

Kilomita moja kutoka ulipo mjengo wa Dodoma kuna uwanja wa Jamhuri. Katazame sehemu ya kuchezea ilivyo mbovu. Yote haya tunayasahau wakati tunapohoji kichapo cha Cairo. Inachekesha sana lakini hakuna jinsi.

Kichapo cha Cairo kimebebwa na historia kubwa nyuma yake. Yale ni mavuno tu yanayotokana na misingi mibovu tuliyoijenga na tunayoendelea kuijenga kila siku sio katika soka tu bali hata michezo mingine. Vigogo hawakujali sana hayo lakini walikwenda Cairo ili warudi na ushindi. Endapo Stars ingeshinda si ajabu wangesema kwamba wao ndio walisababisha timu ishinde.

Pia Soma

Nina matatizo na Amunike katika baadhi ya maeneo, lakini sio kila mmoja anaweza kujigeuza kuwa Jose Mourinho. Kuna maeneo mengi hatujatimiza wajibu kabla ya kuanza kutafuta umaarufu kupitia Taifa Stars. Kule Cairo tunavuna tulichopanda. Moja kati ya misingi mizuri ya matokeo ilipaswa kuwekwa Dodoma miaka mingi iliyopita.

Hata hii Taifa Stars yenyewe kwa kiasi kikubwa mzigo umebebeshwa pale TFF. Tuna tabia ya kuwapokea wanamichezo waliofanya vizuri nje ya nchi na wakati mwingine tunawapeleka bungeni. Ukichunguza, hawakupatiwa msaada mkubwa huko nyuma.

Columnist: mwananchi.co.tz