Ukizungumzia kwenda na wakati basi juua kwa sasa raba zilizopewa jina la ‘Dad Ugly Sneakers’ ndio zinahit sana kitaani hasa kwa mastaa… Karibu katika ulimwengu wa mitindo hapa Bongo5.
Katika ulimwengu huu wa mitindo watu wengi wanapenda kwenda na wakati kwa kuvaa vitu vilivyo na majina makubwa. Mfano:- bidhaa za Louis Vuitton, Balenciaga, Zara na nyinginezo. Ila tokea kuingie trend ya viatu vilivyopewa jina la ‘Dad Ugly Sneaker’ basi baadhi ya mastaa wameamisha mapenzi yao huko.
Unaweza kuhoji kwa nini viatu vimepewa jina hilo, hii ni kwa sababu ya kuonekano wake kuwa mbaya yaani hauvuti. Watu kama Kim Kardashian, Jade Smith, Bella Hadidi na wengineo wameshatinga raba hizi na ku-roll nazo kitaani.
Swali ni Bongo wapo tayari kutinga kitaani na raba hizi zenye muonekano mbaya ila zina trendi?