Kijamii

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Lifestyle

SIL

MenuKijamiiMaoni
Articles

Nanai awapa somo wanafunzi Udom

61797 Nanaipic

Sun, 9 Jun 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dodoma. Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mwananchi Communication Limited (MCL), Francis Nanai amewataka wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) kujipanga kwa maisha wanayoyataka baadaye.

Nanai ameyasema hayo leo Jumamosi Juni 8, 2019 katika ukumbi wa Chimwaga  wakati akizungumza katika warsha ya kujadili maendeleo ya kitaaluma chuoni hapo  iliyowashirikisha pia wahitimu wa miaka nyuma walio katika ajira na waliojiari.

Katika warsha hiyo iliyokuwa na kauli mbiu ya maendeleo ya kitaaluma mara baada ya kumaliza masomo ya sayansi Udom Nanai amesema, "Lazima upange katika maisha yako unataka kuwa  nani? Na baada ya miaka mingapi unataka uwe umefika hapo. Na utengeneze njia ya kufikia hapo."

Amezitaja njia za kutengeneza katika kujipanga maisha unayotaka ni pamoja na elimu, uwezo wa kujieleza na kuwa na tabia nzuri.

“Tunapoajiri tukishaangalia vyeti, tunaangalia nini hasa kinakutofautisha na wengine. Tunaangalia  tabia ukiwa na tabia mbovu huwezi kupata ajira ,”amesema Nanai aliyekuwa akiwasilisha mada ya maendeleo ya taaluuma na ujasiriamali.

Rais wa wanafunzi katika chuo hicho, John Bosco amesema ni vyema mafunzo hayo yakatolewa wakati wanapoanza mwaka wa kwanza ili kujiandaa mapema.

Pia Soma

"Kuna wengine wanasoma masomo ambayo hawakuyapenda na ndio maana unakuta wamesoma masomo ya sayansi wanaenda kuwa wanasiasa," amesema.

Columnist: mwananchi.co.tz