Kijamii

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Lifestyle

SIL

MenuKijamiiMaoni
Articles

MAONI: Shughuli za maendeleo zisiathiri uhifadhi wa mazingira

75130 Peter+elias

Tue, 10 Sep 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Katika miaka ya hivi karibuni, kumekuwa na mjadala mkubwa duniani kuhusu uhifadhi wa mazingira na utekelezaji wa miradi ya maendeleo, ambayo kwa namna moja au nyingine inaharibu mazingira na viumbe vilivyomo ndani yake.

Wanaharakati wamekuwa wakionya juu ya athari za uharibifu wa mazingira unaotokana na miradi ya maendeleo ambayo inasababisha mabadiliko ya tabianchi.

Hata hivyo, wanakubali kwamba siyo vibaya kufanya miradi ya maendeleo bali tahadhari za kimazingira hazina budi kuzingatiwa.

Suala la mabadiliko ya tabianchi na matokeo yake, ni miongoni mwa mambo ambayo yameuamsha ulimwengu kutafakari juu ya mustakabali wa maisha ya kesho, badala ya kufikiria mambo ya leo tu na kuangamiza vizazi vijavyo.

Kwa bahati mbaya, madhara ya uharibifu wa mazingira yanaonekana muda mfupi tu na binadamu wanaoishi sasa ndiyo wanaoumia na athari hizo kama vile hali ya jangwa, mafuriko, ongezeko la joto na kukosekana kwa chakula.

Mazingira na maendeleo ni mambo muhimu ambayo jamii zinatakiwa kuyakumbatia, lakini swali la kujiuliza ni namna gani tunaweza kuhifadhi mazingira wakati huohuo tukiendelea na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo?

Pia Soma

Columnist: mwananchi.co.tz