MAONI: Shughuli za maendeleo zisiathiri uhifadhi wa mazingira
Tuesday September 10 2019
Wanaharakati wamekuwa wakionya juu ya athari za uharibifu wa mazingira unaotokana na miradi ya maendeleo ambayo inasababisha mabadiliko ya tabianchi.
Hata hivyo, wanakubali kwamba siyo vibaya kufanya miradi ya maendeleo bali tahadhari za kimazingira hazina budi kuzingatiwa.
Suala la mabadiliko ya tabianchi na matokeo yake, ni miongoni mwa mambo ambayo yameuamsha ulimwengu kutafakari juu ya mustakabali wa maisha ya kesho, badala ya kufikiria mambo ya leo tu na kuangamiza vizazi vijavyo.
Kwa bahati mbaya, madhara ya uharibifu wa mazingira yanaonekana muda mfupi tu na binadamu wanaoishi sasa ndiyo wanaoumia na athari hizo kama vile hali ya jangwa, mafuriko, ongezeko la joto na kukosekana kwa chakula.
Mazingira na maendeleo ni mambo muhimu ambayo jamii zinatakiwa kuyakumbatia, lakini swali la kujiuliza ni namna gani tunaweza kuhifadhi mazingira wakati huohuo tukiendelea na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo?
Pia Soma
- UCHAMBUZI: Maadhimisho ya Kitaifa Kiswahili na Utamaduni yachochee fursa za kiuchumi
- Askari Polisi, JWTZ kizimbani wakidaiwa kuiba mafuta ya ATCL
MAONI: Shughuli za maendeleo zisiathiri uhifadhi wa mazingira
Tuesday September 10 2019
Wanaharakati wamekuwa wakionya juu ya athari za uharibifu wa mazingira unaotokana na miradi ya maendeleo ambayo inasababisha mabadiliko ya tabianchi.
Hata hivyo, wanakubali kwamba siyo vibaya kufanya miradi ya maendeleo bali tahadhari za kimazingira hazina budi kuzingatiwa.
Suala la mabadiliko ya tabianchi na matokeo yake, ni miongoni mwa mambo ambayo yameuamsha ulimwengu kutafakari juu ya mustakabali wa maisha ya kesho, badala ya kufikiria mambo ya leo tu na kuangamiza vizazi vijavyo.
Kwa bahati mbaya, madhara ya uharibifu wa mazingira yanaonekana muda mfupi tu na binadamu wanaoishi sasa ndiyo wanaoumia na athari hizo kama vile hali ya jangwa, mafuriko, ongezeko la joto na kukosekana kwa chakula.Mazingira na maendeleo ni mambo muhimu ambayo jamii zinatakiwa kuyakumbatia, lakini swali la kujiuliza ni namna gani tunaweza kuhifadhi mazingira wakati huohuo tukiendelea na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo?
Pia Soma