Sun, 24 Nov 2019
Chanzo: mwananchi.co.tz
Anti samahani, kuna kijana anataka kuniposa lakini umbile lake linaniogopesha. Ni mwembamba na hana makalio. Wengi husema wanaume wenye maumbo hayo wanakuwa na maumbile makubwa. Mimi ni mwoga sana, ikiwa hivyo nitashindwa.
Nifanyeje ili nijue kabla hajanioa?
Nimemaliza mwaka sijaonana na mpenzi wangu. Kuna mwanamke nataka awe rafiki yangu wa kimapenzi na nimeshamweleza hilo mara kadhaa na akanikubalia, lakini natimiza mwaka sasa sijaonana naye zaidi ya kuzungumza kwenye simu. Vitendo vyake vinaashiria hanipendi, lakini nikizungumza naye kwenye simu anasisitiza kuwa ananipenda na mimi ni wake wa daima. Nifanyeje?
Hujaniambia anaishi wapi, ila nahisi ni Makka au Madina ambako unahitaji fedha nyingi kama gharama ya usafiri. Kama kweli unampenda na anaishi hapahapa nchini, si ujipange uende kuonana naye? Ukifanya hivyo, ndiyo utajua mbivu na mbichi. Husikii watu wakilalamika kuwa simu zinadanganya? Utaamini vipi maneno wakati huoni vitendo wala mhusika humuoni, kama ameolewa? Jiongeze. Sifa ya mwanaume ni kujiongeza siku zote. Ukikalia kulalamika kuwa anakupenda kwa maneno, atakupenda kweli kwa mtindo huo hadi unazeeka. Nenda kajionee mwenyewe kama ni wako au wa wenzako unashirikiana nao kumtunza. Wengine hulalamika kuuziwa mbuzi kwenye gunia, lakini wewe unajiuzia mwenyewe mbuzi kwenye gunia.
Columnist: mwananchi.co.tz